Jinsi ya Kuishi Maisha Kama Mkristo
Vile tulisema pale mwanzo kwa kitabu hiki Mkristo ni mtu ambaye ameamua kuishi maisha ya kumfuata Yesu na mpango wake kwa maisha yetu. Kuna njia mbili ya kujifunza kufanya hivi:
- Kusoma na kusikiliza mahubiri na mafundisho kutoka kwa maneno ya Yesu ndani ya akanti nne za injili za maisha ya Yesu.kusikiliza mafundisho ya injili ya Yesu ni njia moja nzuri ya kutajirisha maisha yako ya kiroho LAKINI HAKUNA MBADALA YA KUSOMA BIBILIA wewe mwenyewe.
- Soma na usikilize mafundisho na mahubiri kutoka kwa barua ya Paulo na barua za wengine zilioandika katika agano jipya, lakini tena hakuna mbadala ya kusoma na kujifundisha Biblia wewe mwenyewe.
Mzabibu na Matawi
Ni vigumu kuchagua mojawapo hata chache ama mafundisho ya Yesu kuwa mazuri zaidi ama ya muhimu sana kusoma. Injili ya Yesu kwa mlima wa Msaituni (ambapo anafundisha mambo yanayoitea heri- Mathayo 5 na Luka 6) ni kifungu watu wengi wanakijua kama wanajua mafundisho ya Yesu yeyote. Nimezoea kifungu katika kitabu cha Yohana.
- Yohana 15:1-17 - Mtazamo bora maisha ya mkristo
Upendo Mkuu wa Aina Hii
Baada ya kuongoka kwake Kwa miujiza Paulo wa Tarso alikuwa mhubiri aliyefikia watu wengi pia alikuwa mwandishi mashuhuri. Kwa barua yake Kwa wakristo walioishi Korintho (Ugiriki) alionyesha mtindo wa kutojipenda hii Ni tabia ambayo inafaa kuwa na kila Mkristo.
- 1 Korintho 13:1-13- Tabia ya Mkristo
Kubadilisha Mawazo Yetu
Paulo anatuambia katika kitabu cha Warumi (12:2) tusifanane sura ya dunia lakini tubadilishwe kwa kuhuisha mawazo yetu. Katika barua yake kwa wakristo walioko Filipi (Ugiriki) alituonyesha vile tutatimiza hili:
- Wafilipi 4:8 - inaongoza mawazo yetu
Matunda Ya Roho
Katika Yohana 15 Yesu anasema kuhusu kumtii ndio tukaweza kuzaa matunda mengi. Katika barua yake kwa Wakristo walioko Galatia (mjii sasa unaitwa Uturuki) Paulo anaonyesha dhamira ya watu ambao wamejitolea kuishi katika roho:
- Wagalatia 5:22-26 - maisha yaliyoongozwa na roho.
Kusudi la shida
Yesu alitufundisha na barua zote za mitume zinatibitisha kuwa lazima tutarajie shida katika maisha yetu; kuwa mkristo sio ngao ya kuebuka na shida watu hupitia katika maisha. Katika kitabu cha Yakobo anatupa mtazamo mpya wa kuona shida zetu. Wanaweza kuwa ni nafasi kubwa ya kukua.
- Yakobo 1:2-4 - Furahi katika shida zako!
Kukua katika Imani yako
Mitume Petro aliandika barua mbili ambazo zimenakiriwa katika agano jipya. Katika barua yake ya pili anainyesha jinsi na mwenendo wa kukua Imani kwa Mungu.
- 2 Petro 1:3-8 - Kuwa mfuasi mwenye matokeo na mwenye ufanisi wa Yesu
